Machapisho

TUMIENI TAALUMA ZENU KUTATUA CHANGAMOTO ZA MASUALA YA CHAKULA NA LISHE KWENYE JAMII.

Picha
Na Mwandishi wetu-TFNC Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt. Germana Leyna, amefungua mafunzo elekezi kwa Waajiriwa wapya wa Taasisi, ambapo amewataka kutumia taaluma zao katika kusaidia kutatua changamoto mbalimbali za masuala ya chakula na Lishe zinazoikabili jamii. Dkt. Germana amesema mafunzo hayo ya siku tano yamelenga kuwawezesha waajiriwa hao kujua mifumo mbalimbali ya kiutumishi, itakayowasaidia katika kutatua changamoto hizo, na kutekeleza majukumu mbalimbali ambayo Taasisi imekabidhiwa na Serikali kuyatekeleza. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt. Germana Leyna, akitoa maagizo  mbalimbali kwa waajiriwa wapya wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo elekezi   kuhusu sheria, kanuni na taratibu mbalimbali za utumishi wa umma. “Mimi Matarajio yangu kwenu ni makubwa sana, mnisaidie kutatua changamoto za chakula na lishe kwa jamii na ndiyo changamoto ambazo sisi ...

FEDHA ZA WADAU WA MAENDELEO ZITUMIKE KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANANCHI.

Picha
Na. WAF, Dar Es Salaam Watalamu wa Afya nchini, wametakiwa kuwa wazalendo katika kusimamia fedha zinazotolewa na  wadau wa maendeleo, ili kuhakikisha wanatatua  changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi kama ilivyo adhma ya Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.  Wito huo  umetolea Jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Afya Dkt.Godwin Mollel  mara baada ya kufunga  kikao kazi cha tathmini ya namna Tanzania ilivyoweza kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa UVIKO-19. Dkt. Mollel amebainisha  kuwa  wadau wengi wamekuwa wakileta fedha nyingi kwenye sekta ya afya, lakini fedha hizo zimekuwa hazitumiki ipasavyo katika kusaidia sekta hiyo, huku nyingine zikiishia kutumika katika semina na makongamano na kupelekea kushindwa kuwanufaisha wananchi ambao ndiyo walengwa.  “Zinakuja fedha nyingi kutoka kwa wadau, lakini tukishuka chini katika ngazi ya msingi hatuoni matokeo chanya, tuige mfano wa Mhe. Rais  Dkt. Sa...

MWENYEKITI BODI YA USIMAMIZI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WATUMISHI WA TAASISI

Picha
 MATUKIO KATIKA PICHA Watumishi wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania, wakiwa katika kikao cha pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi ya Taasisi Bw.Obey Assery (hayupo pichani) ambapo leo Septemba 14, 2023, anazungumza na Menejimenti na Watumishi kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo mikakati ya namna ya kuiwezesha Taasisi kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kuleta tija kwa taifa. Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania  Bw. Obey Assery, akizungumza na Menejimenti na Watumishi wa Taasisi ( hawapo pichani) ambapo leo amekutana na kuzungumza na watumishi na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu mustakabali wa Taasisi. Afisa Rasilimali Watu wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Maurice Nchimbi, akiwasilisha taarifa ya Utumishi kwa  kwa Mwenyekiti  wa Bodi ya Usimamizi wa Taasisi (hayupo pichani), wakati wa kikao chake na Menejimenti na Watumishi wa Taasisi. Katibu wa Wanawake wa  RAAWU tawi la Taasisi ya Chakula na Lishe Tnzania...

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA AFYA NA MASUALA YA UKIMWI YAZURU TFNC

Picha
  Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Bw. Obbey Assery akizungumza wakati ziara hiyo na kutoa rai kwa wabunge kulisemea suala la lishe katika ngazi ya Taifa (Bungeni,) na katika ngazi ya Halmashauri kupitia mabaraza ya madiwani.Ziara hiyo imefanyika Septemba 12, 20 viongozi wa Taasisi ya Chakula na Lishe (hawapo pichani) baada ya  na Lishe Tanzania ikiwa ni ziara ya kujifunza na kuona shughuli mbalimbali zinazofanywa na Taasisi hiyo. Leo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt. Germana Leyna akitoa mada kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI iliyotembelea Taasisi hiyo kwa lengo la kujifunza na kuona shughuli zinazofanywa na taasisi hiyo. Leo jijini Dar es Salaam. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI wakiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania mara baada ya kuhitimisha ziara hiyo, Leo jijini Dar es Salaam.

WEKENI KIPAUMBELE KWENYE UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE.

Picha
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI imetoa wito kwa Serikali kuendelea kuweka kipaumbele katika utekelezaji wa afua mbalimbali za lishe nchini, ili kuwezesha kuwa taifa lenye watu wenye afya na lishe bora na kuweza kufikia malengo endelevu. Wito huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI, Mhe. Stanslaus Nyongo (MB) baada ya kufanya ziara katika Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania ili kujifunza na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Taasisi hiyo. Mhe.Nyongo amesema afua za lishe zinahitaji kuwa na uwekezaji wa kutosha na kupewa kipaumbele, kwani usipowekeza kwenye lishe unaweza kujikuta unatibu wananchi wengi kwa sababu ya lishe mbovu, wakati unaweza kutumia lishe kama tiba namba moja na yenye gharama nafuu. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIWMI wakipata maelezo kutoka kwa wataalamu wa Maabara ya Chakula na Lishe Tanzania iliyopo Mikocheni, ikiwa ni ziara ya kujifunza na...

VYOMBO VYA HABARI ENDELEENI KUTOA ELIMU YA UNYONYESHAJI MAZIWA YA MAMA

Picha
Na. Mwandishi Wetu- DSM Imeelezwa kuwa vyombo vya habari vinamchango mkubwa katika kutoa taarifa sahihi kuhusu unyonyeshaji na ulishaji wa watoto kwa ujumla na kusaidia kupambana na imani potofu kuhusu unyonyeshaji na taarifa zisizo sahihi zinazolenga maslahi ya kibiashara ya maziwa mbadala na vyakula vya watoto wachanga na hivyo kuchangia uboreshaji wa lisha na afya ya mama na mtoto na kujenga taifa lenye nguvu imara na yenye tija. Hayo yamebainishwa na Mkurungezi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt. Germana Leyna, wakati wa semina elekezi kwa waandishi wa habari mkoa wa Dar es Salaama, kuhusu umuhimu wa kuandika, kuhabarisha na kuelimisha jamii kuhusu masuala mbalimbali yanayohusiana na lishe na afya ikiwa ni mwendelezo wa shughuli mbalimbali zinazofanyika katika kuadhimisha Wiki ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama Duniani. Mkurungezi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt. Germana Leyna (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), wakat...