WAAJIRI WAHIMIZWA KUWASAIDIA WANAWEKA KUNYONYESHA WATOTO HUKU WAKIENDELEA NA KAZI.

 

WAAJIRI WAHIMIZWA KUWASAIDIA WANAWEKA KUNYONYESHA WATOTO HUKU WAKIENDELEA NA KAZI.

 

Naibu waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amefungua rasmi Maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji maziwa ya Mama kitaifa kwa mwaka 2023, ambapo amewahimiza waajiri katika sekta rasmi na zisizo rasmi na jamii kwa ujumla, kuwasaidia wanawake waweze kunyonyesha watoto wao huku wakiendelea kufanya kazi. 

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo Naibu Waziri Dkt. Mollel amesema Maadhimisho ya Mwaka huu yamebebwa na kauli mbiu isemayo “ Saidia Unyonyeshaji: Wezesha Wazazi Kulea Watoto na Kufanya Kazi Zao za Kila Siku” kauli mbiu mbiu ambayo  imelenga kuwawezesha wanawake wote wanaofanya kazi katika sekta rasmi na zisizo rasmi kuweza kunyonyesha na kutunza watoto wao ipasavyo.

Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel akizungumza na wadau wa masuala ya lishe (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi rasmi wa Wiki ya Unyonyeshaji maziwa ya Mama kitaifa kwa mwaka 2023.


Aidha Dkt. Mollel amewakumbusha  Viongozi, Wasimamizi, Watalaam na Watendaji waliopo kuendelea kuelimisha umma kuhusu sheria ya kulinda haki za Uzazi kwa wanawake, kuimarisha, kuwezesha na kujulisha umma mifano na hatua za kuigwa zinazochukuliwa  na wadau kwa lengo kuwasaidia wanawake kuendelea kunyonyesha watoto mahali pa kazi.

 

Akitoa salamu za kwa niaba ya Wadau wa Lishe nchini, mwakilisho kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto Duniani (UNICEF) Patric Codjie,  amesema Shirika hilo  limekuwa mstari wa mbele   kushiriki,  kuendeleza na kufanikisha unyonyeshaji kwa wanawake na litaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kuwawezesha wanawake walioajiriwa kwenye sekta rasmi na zisizo rasmi wanapata wasaa wa kumpa mtoto mwanzo bora kupitia unyonyeshaji.

 

Nchini Tanzania maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji maziwa ya mama yalianza kuadhimishwa mwaka 1992, ambapo huambatana na shughuli mbalimbali zinazolenga kufikisha taarifa, jumbe na hamasa kwa wananchi kuanzia ngazi ya Mkoa, Halmashauri na kwenye jamii.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MATOKEO YA UTAFITI WA HALI YA LISHE YA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI YATOLEWA

TFNC YAIBUKA MSHINDI WA JUMLA MAONESHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI.

WANAFUNZI WANYWE MAZIWA SHULENI-UMMY MWALIMU.