TFNC-KUENDELEA KUSHIRIKIA NA WADAU UTEKELEZAJI AFUA MBALIMBALI ZA LISHE

 Na. Mwandishi Wetu –Dar es Salaam

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzani Dkt. Germana Leyna, amesema Taasisi ya Chakula na Lishe itaendelea kushirikiana na wadau  katika masuala mbalimbali  yanayohusiana na lishe, ili kuweza kutekeleza afua  za kilishe kwa pamoja.

Hayo yamebaninishwa Jijijin Dar es Salaam, wakati wa kikao kati ya Mkurungezi Mtendaji wa wa Taasisi ya Chakula na Lishe Dkt. Germana Leyna na Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la SANKU Bw. Felix Brooks-Church, kilichofanyika katika Ofisi za Shirika hilo zilizopo Masaki.

Katika kikao hicho, aidha Dkt. Germana alipata wasaa wa kufahamu juu ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na shirika hilo katika kuimarisha suala la Uongezaji wa virutubisho vya madini na Vitamini katika vyakula, kupitia teknolojia ya mashine zinazofungwa kwenye Mashine za kusanga unga wa Mahindi.


Mkurungezi wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt. Germana Leyna (kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la SANKU ( hayupo pichani) wakati alipotembea ofisi za Shirika hilo, kujifunza na 
kuangalia maendeleo ya utekelezaji wa afua ya urutubishaji unaofanyika katika kwa Viwanda vidogo na vya kati vinavyozalisha bidhaa za unga wa Mahindi

“Serikali ipo pamoja nanyi na sisi kama Taasisi tupo tayari kuendelea kushirikiana na kuwapa ushauri wa kitaalamu ili kwa pamoja tuweze kushirikiana katika kuimarisha lishe za Watanzania” alisema Dkt. Germana.

 Katika Hatua nyingine Dkt. Germana amewapongeza SANKU kwa jitihada zao wanazochukua katika kusambaza teknolojia yao inayotumika katika urutubishaji wa bidhaa za unga wa mahindi, ambapo amesema zimesaidia kuongeza idadi ya Watanzania wanaotumia unga wenye virutubishi vya madini na Vitamini na kusaidia kupunguza idadi ya wananchi wenye upungufu wa virutubishi hivyo muhimu mwilini.

Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la SANKU  Felix Brooks- Church akitoa maelezo kwa Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania ( hayupo pichani) namna wanavyotekeleza majukumu yao katika kuwawezesha wasindikaji wadogo na wa kati wa unga wa mahindi kupata virutubishi, vifungashio na vinyunyizi (Dosifiers) kwa ajili ya kuongeza virutubishi kwenye unga wa mahindi unaozalishwa nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt. Germana Leyna alitembelea Ofisi za shirika la SANKU na kuangalia maendeleo ya utekelezaji wa afua za urutubishaji wa unga wa mahindi unaotekelezwa na viwanda hivyo, ambavyo vimekuwa vikiwezeshwa teknolojia rafiki kutoka kwa Shirika la SANKU.

MWISHO:

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MATOKEO YA UTAFITI WA HALI YA LISHE YA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI YATOLEWA

TFNC YAIBUKA MSHINDI WA JUMLA MAONESHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI.

WANAFUNZI WANYWE MAZIWA SHULENI-UMMY MWALIMU.