WANANCHI KARAGWE NA KILOLO WAPATIWA ELIMU YA LISHE BORA
Jumla ya wananchi 159 wa vijiji vya Omurusimbi wilayani Karagwe na Igunga wilayani Kilolo wamepatiwa elimu ya Lishe ikiwa ni maadhimisho ya siku ya afya na lishe ya kijiji.
Mafunzo hao yametolewa katika vijiji hivyo vya
mikoa ya Kagera na Iringa ikiwa na muendelezo wa maadhimisho hayo kila baada ya
miezi mitatu ambapo huduma mbalimbali za afya na lishe hutolewa kwa wananchi
Elimu hiyo imejumuisha namna ya kuandaa na kula mlo kamili kwa kutumia vyakula vinavyopatikana katika vijiji vyao huku ikilenga kupunguza tatizo la utapiamlo ikiwemo udumavu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.
Vile
vile wananchi hao wamepatiwa elimu ya ulaji wa mlo kamili ili kuepuka utapiamlo
hususan udumavu kwa watoto.
Maoni
Chapisha Maoni