JUKWAAA LA PAMOJA LA TAARIFA NA TAKWIMU ZA LISHE NCHINI SASA LAZINDULIWA RASMI.

JUKWAAA LA PAMOJA LA TAARIFA NA TAKWIMU ZA LISHE NCHINI SASA LAZINDULIWA RASMI.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Bi. Dorothy Mwaluko akibofya kitufe katika Kompyuta mpakato Kuashiria uzinduzi rasmi wa Jukwaa la Pamoja la taarifa na takwimu za Lishe Nchini, Uzinduzi huo umefanyika jijini Dodoma Disemba 17, 2020 katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, aliyesimama kushoto kushuhudia uzinduzi huo ni Mkurugenzi wa Kinga  Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi na kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt Germana Leyna.

Mtaalamu wa Mifumo kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Idara ya Sayansi ya Uandishi wa Kompyuta Henry Kalisti (Mwenye Shati rangi ya Bluu) akimuonesha Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Bi. Dorothy Mwaluko namna mfumo wa jukwaa la pamoja la taarifa na takwimu za lishe nchini namna unavyofanya kazi, mara baada ya kuzinduliwa na katibu mkuu huyo jijini Dodoma Disemba 17, 2020 katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu.

Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi akimwelezea katibu Mkuu ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Bi Dorothy Mwaluko, namna takwimu na taarifa mbalimbali zitakazoingizwa katika jukwaa la pamoja la taarifa na takwimu za Lishe, zitakavyoweza kutumiwa na wadau wa lishe, ambao watahitaji kupatiwa kwa ajili ya matumizi yao.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Bi. Dorothy Mwaluko akizungumza na watendaji wa Serikali ambao wanatakiwa kusimamia jukwaa la pamoja la taarifa na takwimu za lishe nchini (hawapo pichani) namna ambavyo wanaweze kuendesha jukwaa hilo, ambapo amewataka kuwa makini na matumizi ya takwimu hizo zitakazoingizwa kwenye mfumo 






Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MATOKEO YA UTAFITI WA HALI YA LISHE YA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI YATOLEWA

TFNC YAIBUKA MSHINDI WA JUMLA MAONESHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI.

TUMIENI TAALUMA ZENU KUTATUA CHANGAMOTO ZA MASUALA YA CHAKULA NA LISHE KWENYE JAMII.