WAANDISHI WA HABARI TUMIENI KALAMU ZENU KUANDIKA KWA WINGI HABARI ZA LISHE.
WAANDISHI WA HABARI TUMIENI KALAMU ZENU KUANDIKA KWA WINGI HABARI ZA LISHE.
NA
MWANDISHI WETU
Wito umetolewa kwa Waandishi wa habari kutumia kalamu zao kuandika
kwa wingi habari zinazohusiana na masuala ya Lishe na Afya ili kuweza kubadili
mitazamo na tabia za jamii zilizopo kuhusu masuala ya Lishe na kuweza kuleta
ufanisi katika kupambana na Utapiamlo na Kujenga Taifa lenye Watu wenye Afya
Bora.
Hayo yamebainishwa mkoani Shinyanga na Mganga Mkuu Dkt. Yudas
Ndungile wakati akifungua Semina ya Waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa Lishe
katika kuimarisha Kinga Dhidi ya Magonjwa, ambayo imeratibiwa na Taasisi ya
Chakula na Lishe Tanzania kwa Kushirikiana na Shirika lisilo la Kiserikali la
World Vision Tanzania.
Dkt. Yudas amesema waandishi ni miongoni mwa wadau wakuu wa
mawasiliano yanayolenga kubadili mitazamo na tabia za jamii kuhusu masuala ya
Afya na Lishe hivyo mafunzo hayo yatasaidia kuwajengea uelewa mpana zaidi
kuhusu masuala ya lishe hatua itakayowasaidia kuandika taarifa zenye usahihi.
“Sote tunatambua mchango wa vyombo vya habari katika kutoa
taarifa, kuelimisha na pia kuburudisha, Lakini kwa miaka ya hivi karibuni dhima
hiyo imepanuka na kujumuisha masuala ya ufuatiliaji, kupaza sauti za watu wasio
na sauti katika jamii, kusaidia kulinda maslahi ya jamii na mambo mengine
mengi, hivyo wanahabari wanaweza kuendelea kuhabarisha, kuelimisha kuhusu
umuhimu wa lishe katika kuimarisha kinga dhidi ya magonjwa” alisema Dkt. Dkt.
Yudas
Kwa upande wake
Mkurugenzi wa Elimu ya Lishe na Mafunzo wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania
Sikitu Kihinga alisema mafunzo hayo yanakuja katika wakati ambao Taasisi ya
Chakula na Lishe imeendelea kujikita zaidi katika kushirikiana na wanahabari
kwa kuhakikisha wanajengewa uwezo na kuwa wabobezi katika kuandika habari za
zinazohusu masuala ya lishe
Sikitu alisema wameamua kushirikiana na shirika
la World Vision Tanzania, kwani wao pia ni wadau wakubwa wanaosimamia suala la
lishe, na wamekuwa mstari wa mbele katika kupambana na Utapiamlo na Udumavu ili
kwenda sambamba Serikali katika kufkia malengo iliyojiwekea katika kupambana
magonjwa hayo.
Waandishi
wa habari wa mkoa wa Shinyanga waliojitokeza kushiriki semina juu ya
umuhimu wa lishe katika kuimarisha kinga dhidi ya Magonjwa, wakifuatilia
mafunzo ambayo yametolewa na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania kwa
kushirikiana na World Vision Tanzania
Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania kwa
kushirikiana na World Vision Tanzania mbali na kutoa mafunzo haya kwa
wanahabari wa mkoa wa Shinyanga pia wanatarajia kuyafanya kwa waandishi wa
habari katika mkoa wa Singida, ili kuweza kuwajengea uwezo nao katika kuandika
habari zinazohusiana na masuala ya Chakula na Lishe.
Maoni
Chapisha Maoni