JAMII YAHIMIZWA KUSAIDIA MAJUKUMU YA KAZI MAMA ANAYENYONYESHA KUEPUSHA UTAPIAMLO KWA WATOTO

JAMII YAHIMIZWA KUSAIDIA MAJUKUMU YA KAZI MAMA ANAYENYONYESHA KUEPUSHA UTAPIAMLO KWA WATOTO

Na, TFNC Muheza


ULISHAJI usio sahihi unaochangiwa na mama kuelemewa na majukumu mengi ya kazi na hivyo kukosa muda wa kutosha wa kumtunza mtoto ni sababu kubwa ya utapiamlo kwa watoto.

Hayo yamesema leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji ambayo kitaifa yamefanyika wilayani Muheza mkoani Tanga

"Ni dhahiri kuwa mchango wa mwanamke katika familia, ajira na uzalishaji kwa ujumla ni mkubwa hivyo ni muhimu kuwatia moyo na kuwasaidia wanawake ili waweze kufanya majukumu ya uzalishaji  na utunzaji wa familia kwa ukamilifu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji wa Maziwa ya Mama Duniani (hawapo Pichani) ambayo kwa mwaka huu uzinduzi kitaifa umefanyika wilayani Muheza mkoani Tanga.Picha na Jackson Monela

Waziri Ummy amesema kuwa jamii ina wajibu wa kuwawezesha wazazi, hususani wanawake waweze kunyonyesha watoto wao maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya mwanzo baada ya kujifungua.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, akimkabidhi Mwakilishi wa  Chama cha Waandishi wa Habari mkoa wa Tanga Burhan Yakubu kitini cha Lishe ya wanawake, Watoto na Vijana Balehe kwa ajili ya Vyombo vya Habari, kuashiria kuanza kutumika rasmi kwa kitini hicho, wakati wa Uzinduzi wa Wiki la Unyonyonyeshaji maziwa ya Mama Duniani, ambayo kwa hapa nchini yamefanyika wilayani Muheza mkoani Tanga.

Aidha, amesema watoto wanapotimiza miezi sita waanzishiwe vyakula vya nyongeza vyenye ubora kilishe huku wakiendelea kunyonyeshwa hadi watakapotimiza umri wa miaka miwili.

Kwa upande wa takwimu za hali ya ulishaji watoto nchini Tanzania zinaonesha kuwa takribani asilimia 97 ya watoto wenyeumri chini ya miaka miwili wananyonyeshwa maziwa ya mama.

"Idadi ya watoto wanaoanzishiwa kunyonyeshwa maziwa ya mama kwa wakati sahihi katika kipindi kisichozidi saa moja baada ya kuzaliwa ni asilimia 53 na idadi ya watoto wanaonyonyeshwa maziwa ya mama pekee bila kupewa maji, vinywaji na vyakula vingine katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo baada ya kuzaliwa ni asilimia 58”, alisema Waziri Ummy.

"Vigezo hivyo ni idadi sahihi ya milo anayopewa mtoto kwa siku kulingana na umri wake, na mlo uwe na mchanganyiko wa vyakula kutoka kwenye makundi yasiyopungua manne ya vyakula," amesisitiza.

Amesema Maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji Duniani kwa mwaka 2020 yamebebwa na kauli mbiu inayosema “Tuwawezeshe wanawake kunyonyesha watoto kwa afya bora na ulizni wa mazingira"

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MATOKEO YA UTAFITI WA HALI YA LISHE YA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI YATOLEWA

TFNC YAIBUKA MSHINDI WA JUMLA MAONESHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI.

WANAFUNZI WANYWE MAZIWA SHULENI-UMMY MWALIMU.