WAZAZI NA WALEZI MSIOGOPE KUTUMIA VIRUTUBISHI MCHANGANYIKO KWENYE VYAKULA VYA WATOTO WENU.

WAZAZI NA WALEZI MSIOGOPE KUTUMIA VIRUTUBISHI MCHANGANYIKO KWENYE VYAKULA VYA WATOTO WENU.

Na, Jackson Monela, TFNC

Wazazi na Walezi katika Wilaya za  Ikungi na Manyoni wametakiwa kuachana na imani potofu kuwa virutubisho mchanganyiko vina madhara kwa Watoto, na kuhofia kuvitumia, ilhali vimekuwa na msaada mkubwa katika kusaidia ukuaji mzuri wa mtoto na kusaidia katika kupambana na udumavu.

Wito huo umetolewa Mkoani Singida  na Mkurugenzi wa Elimu na Mafunzo ya Lishe  kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Bi.Sikitu Kihinga, wakati wa mafunzo kwa watoa huduma za afya  wa Halmashauri hizo, juu ya  matumizi ya Virutubisho mchanganyiko ambavyo hutolewa kwa Watoto wenye umri wa miezi 6 hadi 23.

Sikitu amesema Virutubisho mchanganyiko vina umuhimu mkubwa sana kwa watoto kwani vinasaidia kupambana na tatizo la udumavu, ikizingatiwa katika jamii  nyingi kumekuwa na changamoto baadhi ya wazazi na walezi kushindwa kuandaa mlo unaokidhi mahitaji yote ya virutubishi vinavyohitajika kwa mtoto.

Washiriki wa mafunzo ya matumizi ya virutubishi mchanganyiko wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mafunzo hayo yalifanyika kuanzia tarehe 15 hadi 17 Juni 2020 katika halmashauri za IKungi na Manyoni mkoani SINGIDA.

Halmshauri za Ikungi na Manyoni zipo kwenye  utekelezaji wa mradi wa ugawaji virutubisho mchanganyiko kwa Watoto wenye umri wa miezi 6 hadi 23, ukiwa chini ya Ufadhili wa Shirika la Nutrition  International na kusimamiwa na Shirika la World Vision, ambapo mpaka kufikia mwezi Machi 2020 katika halmashauri hizo mbili jumla ya Watoto 16416 wamefikiwa na huduma hiyo

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MATOKEO YA UTAFITI WA HALI YA LISHE YA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI YATOLEWA

TFNC YAIBUKA MSHINDI WA JUMLA MAONESHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI.

WANAFUNZI WANYWE MAZIWA SHULENI-UMMY MWALIMU.