UMMY MWALIMU: TUTANDELEA KUTOA AJIRA KWA WAUGUZI NCHINI
UMMY
MWALIMU: TUTANDELEA KUTOA AJIRA KWA WAUGUZI NCHINI
Na,
WAMJW
Serikali
imesema itaendelea kutoa kipaumbele katika ajira za wauguzi kadri nafasi
zitakavyokuwa zikipatikana ili kuboresha huduma za afya nchini.
Kauli
hiyo imetolewa leo na Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akizungumza na
watumishi wa hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika Maadhimisho ya
Siku ya Waguzi Duniani ambayo
huadhimishwa tarehe 12 Mei kila mwaka. Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Wauguzi;
Sauti inayoongoza Uuguzi kwa Dunia yenye Afya.”
Waziri
Ummy Mwalimu amesema Serikali itaendelea kutoa kipaumbele katika ajira za
wauguzi kwa sababu kuna uhaba wa wauguzi kwenye vituo vya afya licha ya kuwapo
zaidi ya wauguzi 30,451 katika vituo vya umma na binafsi nchini.
Amesema
asilimia 80 ya huduma za afya katika
vituo vya kutoa huduma za afya zinatolewa na wauguzi hivyo Serikali itaendelea
kutambua na kuthamini kazi nzuri zinazofanywa na wauguzi nchini.
“Wauguzi wamekuwa wapambanaji wakubwa katika
kutoa huduma kwa washukiwa wa ugonjwa wa Corona (Covid-19), hivyo
hongereni wauguzi wote nchini Tanzania,”
amesema Waziri.
Amesema
katika jitihada za Serikali za kuboresha huduma za wauguzi na wakunga, Serikali
imekamilisha muongozo wa kutoa huduma kwa kuzingatia utu, heshima na maadili.
Waziri
wa Afya amesema jumla ya waguzi 778 katika hospitali 15 za rufaa za mkoa
wamepatiwa mafunzo muhimu ili kuwezesha mpango wa kutoa huduma rafiki kwa
wananchi na kwa kujali utu wao.
“Mafunzo haya yataendelea kutolewa katika ngazi zote za kutoa huduma na tayari tumetengeneza mfumo wa kupokea taarifa za malalamiko na kero kutoka kwenye vituo vya kutolea huduma,” amesema Waziri Ummy Mwalimu.
Naye Rais wa Chama cha Wauguzi na Wakunga Tanzania (TANNA), Bw. Alexander Baluhya amesema ili kuwapo kwa huduma bora na salama za afya, nchi inapaswa kuwa na wataalamu wenye weledi wa hali ya juu na mazingira bora ya kazi.
“Hivi sasa nchi yetu ina wauguzi 30,451 waliojiriwa katika sekta ya afya ambao ni takribani asilimia 60 ya wataalamu wote wa afya. Wauguzi hawa wanatoa zaidi ya asilimia 80 ya huduma za afya ambazo zimekuwa zikitolewa kwa Watanzania. Hivyo upungufu wa wauguzi na wakunga ni asilimia 48,” amesema Bw. Baluhya.
Bw.
Baluhya amewapongeza wauguzi nchini
kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maadili ya taaluma yao hasa katika
kipindi hiki cha maambukizi ya virusi vya Corona (Covid-19).
Maoni
Chapisha Maoni