MLONGAZILA YAADHIMISHA MIAKA 200 YA TAALUMA YA UUGUZI

Mloganzila yaadhimisha miaka 200 ya taaluma ya uuguzi

Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila katika kumbukizi ya siku ya wauguzi duniani imewapongeza wauguzi kwa kutoa huduma bora za afya kwa wagonjwa lengo ikiwa ni kuonyesha kuwa inatambua na kuthamini mchango wa wauguzi katika kuihudumia jamii.

Maadhimisho hayo hufanyika Mei 12, kila mwaka ambapo mwaka huu yana kauli mbiu isemayo “Wauguzi sauti inayoongoza kwa dunia yenye Afya”.

Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo, Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Dkt. Julieth Magandi amewapongeza wauguzi kwa kuwa mstari wa mbele kwa kutoa huduma bora za afya huku wakizingatia kanuni na taratibu zilizowekwa na taaluma hiyo.

 “Nawapongeza sana kwa kumbukizi ya miaka 200 ya taaluma ya uuguzi tunatambua na kuthamini mchango wenu kwa kuwa mstari wa mbele katika kutoa huduma huku mkijali utu, taaluma hii ni ya muhimu sana na mnaweza kuwa mmejionea jinsi hospitali inavyoendelea kufadhili masomo kwa wauguzi mbalimbali wanaojiendeleza ili kuboresha utoaji huduma katika hospitali yetu” amesema Dkt. Magandi.

Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Dkt. Julieth Magandi akiwapongeza wauguzi wakati wa maadhimisho ya siku ya wauguzi duniani

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi wa MNH-Mloganzila, Sr. Redemptha Matindi amewaeleza wauguzi kuwa taaluma ya uuguzi ni taaluma inayohitaji upendo, utu, heshima, kujali na kujitoa ili kuwapatia wagonjwa huduma stahiki bila kujali uwezo au uofauti wa kipato.

Katika kuadhimisha siku hii wauguzi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila walikata keki na kuwasha mishumaa ikiwa ni alama ya kuwakumbusha kuendelea kutoa huduma kwa upendo, ukarimu, uvumilivu na kujali utu.

Wauguzi wakiwa wamewasha mishamaa ishara ya upendo, uvumilivu, heshima, ukarimu na kujitoa katika taaluma hiyo.



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MATOKEO YA UTAFITI WA HALI YA LISHE YA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI YATOLEWA

TFNC YAIBUKA MSHINDI WA JUMLA MAONESHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI.

WANAFUNZI WANYWE MAZIWA SHULENI-UMMY MWALIMU.