Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba 11, 2020

TFNC YAIBUKA MSHINDI WA JUMLA MAONESHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI.

Picha
  TFNC YAIBUKA MSHINDI WA JUMLA MAONESHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI 2020. Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga (wa kwanza kushoto) akikabidhi zawadi ya mshindi wa jumla wa maonesho ya maadhimisho ya Siku ya Chakula Duniani kwa mwaka wa  2020 yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe kwa Bi Adeline Munuo kutoka  Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania, mara baada ya Taasisi hiyo kuibuka mshindi wa Jumla katika maonesho hayo yaliyofanyika katika Viwanja vya Lunyanyo mkoani humo. Afisa Lishe Mtafiti Mwandamizi kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Adeline Munuo, akiwa pamoja na wafanyakazi wengine wa Taasisi hiyo, wakishangilia mara baada ya kupokea tuzo ya Ushindi wa jumla ya  Maonesho ya Maadhimisho ya Siku ya chakula Duniani kwa mwaka wa 2020 kutoka kwa Waziri wa kilimo Japhet Hasunga (Mwenye suti nyeusi), ambaye aliitimisha maadhimisho hayo, ambayo kitaifa yamefanyika mkoani Njombe. Afisa Lishe Mtafiti wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Elizabeth Lyimo, akifurahi ushindi wa Taasi
Picha
   TFNC YASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI   Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mghumba (Mwenye skafu) akipokea maelezo ya makundi matano ya vyakula vilivyopo kwenye piramidi ya lishe kutoka kwa Afisa lishe mtafiti mwandamizi Mary Ngilisho wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania,mara baada ya naibu waziri kutembelea banda la Maonyesho la Taasisi hiyo, wakati wa uzinduzi wa wiki la maadhimisho ya siku ya chakula duniani, ambapo kwa hapa nchini kitaifa yanafanyika mkoani Njombe. Mkuu wa Idara ya Sayansi ya Chakula na Lishe kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt: Elifatio Towo akitoa maelezo kwa naibu waziri wa Kilimo Omary Mghumba namna Taasisi hiyo inavyoshiriki katika uelimishaji na utafiti wa masuala ya Chakula na lishe, mara baada ya Naibu waziri kutembelea banda la Maonyesho la Taasisi ya Chakula na Lishe mara baada ya kuzindua Maadhimisho ya Siku ya Chakula Duniani ambayo Kitaifa yanafanyika mkoani Njombe. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete Fran