Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba 23, 2020

WAANDISHI WA HABARI TUMIENI KALAMU ZENU KUANDIKA KWA WINGI HABARI ZA LISHE.

Picha
WAANDISHI WA HABARI TUMIENI KALAMU ZENU KUANDIKA KWA WINGI HABARI ZA LISHE. NA MWANDISHI WETU Wito umetolewa kwa Waandishi wa habari kutumia kalamu zao kuandika kwa wingi habari zinazohusiana na masuala ya Lishe na Afya ili kuweza kubadili mitazamo na tabia za jamii zilizopo kuhusu masuala ya Lishe na kuweza kuleta ufanisi katika kupambana na Utapiamlo na Kujenga Taifa lenye Watu wenye Afya Bora. Hayo yamebainishwa mkoani Shinyanga na Mganga Mkuu Dkt. Yudas Ndungile wakati akifungua Semina ya Waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa Lishe katika kuimarisha Kinga Dhidi ya Magonjwa, ambayo imeratibiwa na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania kwa Kushirikiana na Shirika lisilo la Kiserikali la World Vision Tanzania.  Dkt. Yudas amesema waandishi ni miongoni mwa wadau wakuu wa mawasiliano yanayolenga kubadili mitazamo na tabia za jamii kuhusu masuala ya Afya na Lishe hivyo mafunzo hayo yatasaidia kuwajengea uelewa mpana zaidi kuhusu masuala ya lishe hatua itakayowasaidia kuandika taarifa z