Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti 27, 2020

TANZANIA KUANZA KUZALISHA VYAKULA VYA NYONGEZA KWA WATOTO UMRI CHINI YA MIAKA 5.

Picha
TANZANIA KUANZA KUZALISHA VYAKULA VYA NYONGEZA KWA WATOTO UMRI CHINI YA MIAKA 5. NA MWANDISHI WETU Tanzania iko mbioni kuachana na kuagiza vyakula vya nyogeza kwa Watoto kutoka nje ya nchi na matokeo yake vitaanza kuzalishwa hapa hapa nchini, mara baada ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania kwa kushirikiana na MUHAS, SUA na TBS kuja na mradi wa kutengeneza vyakula vya nyongeza kwa ajili ya Watoto chini ya umri wa miaka mitano, ili kuhakikisha wanapata chakula kilichoboreshwa na kinachokidhi mahitaji yao.   Akizungumza wakati wa Uzinduzi wa mradi huo Mkoani Morogoro Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya   Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto   Edward Mbanga kwa niaba ya Waziri wa Afya,     Ummy Mwalimu amesema hadi sasa hakuna hakuna uzalishaji wa kibiashara wa vyakula vya nyongeza hapa nchini na badala yake vimekuwa vikiagizwa kwa wazalishaji mbalimbali kutoka nje ya nchi.   Baadhi ya Viongezi  wa Taasisi zinazoshiriki kwenye mradi wa kutengeneza vyakula

TFNC, KWA KUSHIRIKIANA NA MUHAS, SUA, TBS KWA KUPITIA UFADHILI WA WFP WAZINDUA MRADI WA KUTENGENEZA VYAKULA VYA NYONGEZA KWA WATOTO WENYE UMRI CHINI YA MIAKA 5

Picha
TFNC, KWA KUSHIRIKIANA NA MUHAS, SUA, TBS KWA KUPITIA UFADHILI WA WFP WAZINDUA MRADI WA KUTENGENEZA VYAKULA VYA NYONGEZA KWA WATOTO WENYE UMRI CHINI YA MIAKA 5 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Dk. Germana Leyna akiwasilisha taarifa ya mradi wa Kutengenezaa vyakula vya nyongeza kwa watoto wenye umri chini ya Miaka mitano kwa wadau wa lishe (Hawapo pichani) wakati wa Uzinduzi wa mradi huo mkoani Morogoro, ambao utatekelezwa na Taasisi hiyo kwa kushirikiana na SUA, MUHAS na TBS kupitia ufadhili wa WFP Baadhi ya Viongezi  wa Taasisi zinazoshiriki kwenye mradi wa kutengeneza vyakula vya  nyongeza kwa watoto wenye umri chini ya miakaa mitano, wakiangalia mojawapo ya mashine ambayo itatumika  katika uzalishaji wa vyakula hivyo, mara baada ya kutembelea eneo la kiwanda kitachotumika kuzalisha malighafi zitakazotumika kuandalia vyakula nyongeza, katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine. Makamu Mkuu wa Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Prof. Andrea Pembe akisikiliza